Home Up Feedback Search

Tractor Repairs
Home Up

Soma kipeperushi cha kuhusu mikopo ya pembejeo

       

United Republic of Tanzania, Ministry of Agriculture, Food Security & Corperatives, Agricultural Inputs Trust Fund. AGITF.  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Mfuko wa Pembejeo.

Taratibu na Masharti ya Mikopo ya Kukarabati Matrekta

1. Mwombaji atajaza fomu maalum ya maombi inayopatikana katika Ofisi za kilimo za Halmashauri za Wilaya na Makao makuu y Mfuko wa Pembejeo, jijini Dar-es-salaam.

2. Fomu   za   maombi   zilizojazwa   na kuambatanishwa na vielelezo vinavyohitajika zitapitishwa na kuidhinishwa na Afisa Kilimo na Maendeleo ya Mifugo wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya husika na baadaye kutumwa mapema kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Pembejeo.

3. Mikopo ya kununua matrekta inapitia benki, mwombaji sharti atimize yafuatayo:-

·         Awe na dhamana binafsi kwa jina lake isiyohamishika yenye hati miliki (title deed) na inayokubalika kisheria.

·         Awe tayari kutekeleza masharti ya mikopo ya benki itakayotoa mikopo kwa
niaba ya Mfuko wa Pembejeo ikiwa ni pamoja na kufungua akaunti na benki husika, kulipa asilimia moja (1%) ya mkopo kabla ya mkopo haujaidhinishwa na kutolewa, na kusajili trekta kwa jina lake na benki au taasisi ya fedha itakayotoa mkopo.

·         Awe tayari kulifanyia matengenezo madogo   na   makubwa   trekta litakalonunuliwa kwa mkopo mara kwa mara kama atakavyoelekezwa na mtengenezaji au muuzaji wa trekta hilo.

4. Muda wa mkopo ni miaka mitatu kwa riba ya asilimia kumi (10%)

 

.

 

Send mail to agitf@mari.or.tz with questions or comments about this web site.
Last modified: 03/06/07